Ethiopia   Tanzania   Kenya   Uganda   Mozambique   Madagascar   Malawi   Zambia   Zimbabwe   South Sudan   Rwanda   Burundi   Somalia   Eritrea   Mauritius   Djibouti   Reunion   Comoros   Mayotte   Seychelles DR Congo   Haiti   United  States   Egypt   Ghana   Nigeria   South Africa
LAVA LAVA
Home » KONPA/COMPAS/KOMPA  »  LAVA LAVA
WhatsApp-Image-2024-04-02-at-11.49.36-AM-1

LAVA LAVA

Biography:

Artist/Stage Name: LAVA LAVA

Birth Name/Original Spelling: Abdul Juma Idd

Birthday: March 27, 1993

Country: Kigoma Region, Tanzania

Occupation: Singer * Actor* Writer* Director

Marital:

Partner/Spouse:

Children:

Siblings:

MUSICAL CAREER

Other A.K.A Names:

Origin: Tanzania

Region: East African Artist* Eastern Africa Artist* East Africa Artist*

Languages: Swahili, English

Lyrics: Tukaze Roho* Utatulia*

Genres: Afro Pop*Folk*Bongo Flava* Ndombolo* R&B*Konpa/Compas/Kompa

Instruments: Piano *Vocals

Biography:

Awards: 2

Album/EP:

Videos:

Labels: *WCB Wasafi Record Label

Years Active: 2004- Present *

Artist Site:

EOLLYWOOD* EAEEA-East Afro Entertainment Empire Artistry

EOLLYWOOD* EAEEI-East Afro Entertainment Empire Industry

EOLLYWOOD* EAEEA-East Africa Entertainment Empire Artistry

EOLLYWOOD* EAEEA-East African Entertainment Empire Artistry

LYRICS & VIDEOS

• Habibi
• Utatulia
• Tukaze Roho

Habibi lyrics

Una rangi ya chotara
Manga manga asili ya ki-Zanzibari
Chokoleti colour mixer m-Tanga Tanga
Una ng'ara ng'aring'ari
Ngozi laini kanchori, sambusa bhajia
Upo kama mdoli, yaani kama wa bandia
Eeeh eeh eeeh..
Ukitembea koko (Koko)
Huko nyuma baikoko (Koko)
Mzigo siwabuku ngojero
Sotojo la bokoboko (Boko)
Laini nyanya ya kopo (Kopo)
Yaani bonyero bonyero
Eeeh achana naki naki
Hawana lolote
Watazusha na wajigi jigi
Penzi watie tope
Nikupeleke kwa bibi
Tiffah ama Dangote
Uvae shehe la wigi
Utapata kwa Aristote
Habibi (Habibi)
Nurulhaini kipenda roho (Habibi)
Nyonga mkali haini
Uwooo (Habibi)
Habibi (Habibi)
Nurulhaini kipenda roho (Habibi)
Nyonga mkali haini
Uwooo uwooo
Penzi lisiwe dibaji
Zidisha utamu tende
Mahaba yawe full charge
Tukomeshe visadi viwebe
Nikande kande masaji
Wabaki kupiga vijembe
Wakailiki magadi
Ongeza na peremende (aah)
Mchunge shetwani
Mama twende pole pole (aah)
Kuna Esma, Khan
Akina Juma Lokole (aah)
Wasikupande kichwani
Wakazua mambo ya uchochole (aah)
Iwe aibu mtaani
Insta michambo wanichore
Achana naki naki
Hawana lolote
Watazusha na wajigi jigi
Penzi watie tope
Nikupeleke kwa bibi
Tiffah ama Dangote
Uvae shehe la wigi
Utapata kwa Aristote
Habibi (Habibi)
Nurulhaini kipenda roho (Habibi)
Nyonga mkali haini
Uwooo (Habibi)
Habibi (Habibi)
Nurulhaini kipenda roho (Habibi)
Nyonga mkali haini
Uwooo uwooo
(Ayolizer)
Usije kughairi ghairi
Mi mwingine sina
Usije kughairi ghairi
Penzi likachina
Usije kughairi ghairi
Ukanitosa mazima
Usije kughairi ghairi
Nuru ikazima
(Wasafi)

Tukaze Roho lyrics

Spice music
Maisha yangu si ya ki papa
Ni vitembele ya nyanya chungu
Dagaa kurusungu, hummh
Niko chakavu na nimechakaa
Yaani naishi ki mungu mungu
Mtetezi wa bunjuu
Mjukuu wa binti simba
Okoa mangala
Wa mwisho kitinda mimba
Mwenye elimu uchwara
Maisha yalivyo nifilimba, akanijalia jallah
Nikaanza kuimba, uniondoke ufukara
Ila bado,
Kipato changu cha chini nacho kina utata
Hata visenti hamsini kuvipata mashaka
Nalia na umasikini mungu ashushe baraka
Enyi wezangu na mimi tusikate tamaa
Tukaze roho, tukaze roho tusichoke
Tukaze roho ,mungu wa kwetu sote
Tukaze roho, eeh tusichoke
Tukaze roho, mungu wa kwetu sote
Mmh
Japo, maisha yenye ya manati
Hatupati kila tukilenga
Kukicha misumari ya bati
Kuku kapenya kwa tenga
Kula yetu tu ni wasiwasi
Tutapata wapi ya kujenga
Wa kupiga picha masaai
Kulala mbagala kwa chemba
Tunaunga unga mwana (haya ndo mambo yetu)
Hayana tofauti na jana (ndo maisha yetu)
Wazazi kulala na mwana (heey...)
Chumba kimoja mandoo, masufuria (wenyewe tushazoea)
Kipato changu cha chini, nacho kina utata
Ata visenti hamsini kuvipata mashaka
Nalia na umasikini mungu ashushe baraka
Enyi wezangu na mimi tusikate tamaa
Tukaze roho, tukaze roho tusichoke
Tukaze roho, mungu wa kwetu sote
Tukaze roho, eeh tusichoke
Tukaze roho, mungu wa kwetu sote
(Ayolizer)
Wanangu wa bodaboda, tukaze roho
Kina mama vikoba, tukaze roho
Ah rumbesi wabeba virogha, tukaze roho
Vijana wezangu, tukaze roho
Tutapata tu

Utatulia lyrics

Kiangazi masika ukiichanganya
Vyote vikashuka kwangu vitanielemea
Ntakosa pa kushika ntavavanya
Wewe ndo mwandani wangu nliokuzoea
Ntunza vyangu visiri mwenye kunisitiri
Fundi mitambo
Kinga yangu ya mwili usiyelipa bili
Kuchoma changu
Simtaki kafiri jangiri, mwingi wa mambo
Moyo akaukatilli
Nikondeshe mwili ajifanye rambo
Si unajua
Dalili ya mvua mawingu
Ikitaka kunyesha
Huwa yanatanda
Nami si unanjua aah
Nimeumbwa na wivu
Kidogo tu presha
Yanshuka yapanda
Niahidi kama
(Utatulia aaah)
Baby, niahidi kama
(Utatulia aaah)
Hhhmm nisibaki nkashika tama
(Utatulia aaah)
Baby, niahidi kama
(Utatulia aaah)
Hhhmm wasiniibie cha ngama
Maneno yangu
Si biblia wala masaafu
Useme usibadili hhhmm
Jichunge kipenzi changu
Unanisikia usicheze rafu
Yatimie waliotabiri
Yeah yeah…
Usijifanye Ronaldinho
Penzi utie mbwembwe utahaaribu
Visokolokwinyo wakupitie denge kukujaribu
Kina capachino
Wakakutia wenge kwa vizabibu
Wakugongeshe mvinyo
Ukaota mapembe iwe aibu
Si unajua
Dalili ya mvua mawingu
Ikitaka kunyesha
Huwa yanatanda
Nami si unanjua aah
Nimeumbwa na wivu
Kidogo tu presha
Yanishuka yapanda
Niahidi kama
(Utatulia aaah)
Baby, niahidi kama
(Utatulia aaah)
Hhhmm nisibaki nkashika tama
(Utatulia aaah)
Baby, niahidi kama
(Utatulia aaah)
Hhhmm wasiniibie cha ngama
Eeeh eh yani kama
(ukitulia tulia)
Sitathubutu macho kupepesa
(ukitulia tulia)
Ukinipa kiduchu nitatosheka
(kama ukitulia tulia)
Sitofwata nguruchu niende teseka
(ukitulia tulia)
Eeeh Nami ntatulia